Leo Waziri wa Mambo ya ndani Charles Kitwanga alitembelea ofisi za zimamoto na kujionea changamoto mbalimbali zinazolikabili jeshi la uokoaji.
Uhaba wa vifaa..”Kuna haja ya kutafuta maeneo mengine ya kuweka vifaa, hali ya eneo ya kuhifadhia vifaa halijabadilika, Ni kweli bajeti ni ndogo lakini nimeongea na uongozi kuhakikisha wanakusanya mapato ili kupata vifaa vya kutosha“..
Adhabu kwa madereva wasioheshimu magari ya zimamoto...”Sasa
hivi tunajenga barabara za mabasi yaendayo kasi, tutarahisisha wenzetu
wa zimamoto waweze kupita sehemu hiyohiyo ili waweze kufika haraka
kwenye tukio..Madereva wawe wepesi wa kupisha magari yanayokwenda kwenye
dharura, yawe ya wagonjwa ama yale ya zima moto na wale wanaokiuka
wachukuliwe sheria kali…Kitwanga
Mipango ya kupata vifaa vya kisasa…“Katika
viwanja vya ndege tuna magari ya zimamoto ya kisasa sana, tuhakikishe
tunajipanga vizuri kuhakikisha tunapata vifaa imara na vya kisasa zaidi“..
No comments:
Post a Comment